VIEW OTHER SITES

Monday

KOTOKO YATWAA UBINGWA GHANA

Klabu kongwe nchini Ghana ya Asante Kotoko imefanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu msimu wa 2011/2012 nchini humo hii leo.
Timu hiyo imetwaa ubingwa huo baada ya kuifunga Tema Youth kwa goli moja bila majibu kupitia kwa Richard Yeboah iliyeunganisha krosi ya Kofi Nti_Boakye kutokea wingi ya kushoto dakika ya 57.
Mchezo huo uliopigwa kwenye mji wa Kumasi ulishudiwa na mashabiki lukuki wa Kotoko ambapo beki wa kushoto wa Kotoko, Gideon Baah alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo kutokana na kiwango alichokionesha kwa kuisumbua timu ya Tema Youth.
Kocha wa KOtoko, Maxwell Konadu alimjumuisha Ben Acheampong kwenye kikosi chake hii leo ambaye ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ghana “Black Stars” kitakachoikabili Lesotho mwishoni mwa wiki hii.
Nafasi ya pili imeenda kwa Ashanti Gold iliyofikisha alama 47 baada ya kuifunga Ebusua Dwarfs magoli 2-0 kwenye uwanja wa Sekondi kupitia kwa Mohamed Yakubu.
Matokeo mengine na miji ilikochezwa michezo hiyo,
Accra: Hearts 4-0 Arsenals
Dormaa: Aduana 1-0 Liberty
Wa: A. Stars 1-0 Medeama
Bekwai: New Edubiase 1-0 Bechem Utd
Berekum: Chelsea 1-1 Mighty Jets


MSIMAMO MZIMA BAADA YA KUMALIZA KWA LIGI HIYO HII LEO;
1    Asante Kotoko 30   18   9    3    42   18   24   59
2    AshantiGold FC 30   13   10   7    34   33   1    48
3    Adunana Stars 31   11   14   6    25   15   10   47
4    Hearts of Oak 30   13   10   7    31   19   12   46
5    Medeama SC    30   13   5    12   39   34   5    44
6    Liberty Professionals   30   11   9    10   38   29   9  42
7    Berekum Chelsea    30   11   12   7    30   23   7    41
8    Edubiase FC   30   13   5    12   34   36   -2   38
9    Tema Youth    30   9    9    12   31   30   1    35
10   WA All Stars  30   10   10   10   19   20   -1   34
11   Dwarfs    30   9    10   11   23   25   -2   33
12   Arsenals  31   7    10   14   24   40   -16  31
13   Heart of Lions 30   7    11   12   21   31   -10  29
14   Wassaman United    30   7    8    15   27   42   -15  29
15   Mighty Jets   30   5    14   11   23   29   -6   28
16   Bechem United 30   5    12   13   24   41   -17  27

No comments:

Post a Comment