VIEW OTHER SITES

Friday

KIPLAGAT: SSMB HAIKUPEWA 350 MILIONI NA SERIKALI

Mwenyekiti wa chama cha riadha nchini Kenya (AK), Isaiah Kiplagat amemtaka waziri wa michezo nchini humo, Ababu Namwamba kufuatilia kwa umakini kauli yake kufuatia kauli ya waziri huyo kuwa serikali ya Kenya imetoa shilingi milioni 350 kwa bodi ya usimamizi wa viwanja vya michezo (SSMB).

Kiplagat ambaye ni mjumbe wa bodi hiyo amesema kuwa bodi yake imepatiwa shilingi milioni 70 kwa ajili ya ukarabati wa Kipchoge uliopo Eldoret kutoka kwenye milioni 100 ambazo zilitengwa kwa ajili ya vifaa vya michezo.

Kauli ya waziri huyo imeleta mkanganyiko na bodi hiyo kutokana na ukweli kuwa fedha hizo zilikabidhiwa kwa kitengo cha michezo kinachojihusisha na maendeleo ya miundombinu ya michezo chini ya wizara hiyo na si bodi hiyo.

Kiplagat amesema kuwa waziri wa michezo, Namwamba ameshauriwa vibaya kuhusu zilikopelekwa fedha hizo, na kwamba bodi hiyo imepokea fedha za ukarabati wa viwanja na kuendesha taasisi hiyo tu.

Wawili hao wanadaiwa kukwaruzana wakati wa ufunguzi wa shule ya kukuza vipaji ya Lornah Kiplagat iliyopo Iten, huku Kiplagat akidai kuwa hana mawazo mabaya dhidi ya waziri huyo.

"Waziri hajashauriwa vizuri kuhusu kazi za SSMB na ndio maana alizungumza kitu ambacho hakifahamu," alisema.

Aliongeza kuwa, kwa kaulia ya waziri inamaanisha SSMB haikuumia vizuri fedha hizo kitu ambacho si kweli, na kwamba waziri huyo alitakiwa kupewa taarifa sahihi kuhusu uhusiano uliopo baina ya wizara na bodi hiyo.

Kiplagat alimalizia kwa kusema kuwa hausiki na upotevu wa msaada kamati ya olimpiki ya 2004 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja North Rift, lakini pia akimtaka waziri huyo kutatua matatizo kwa njia ya amani na mazungumzo na si kutumia vitisho

Kiplagat vs Namwamba

TUZO ZA MADJ BORA GHANA FEB. 15

The Ghana DJ Awards will finally come off on February 15, at the National Theatre, the organizers Merqury Republic has said.

Originally scheduled to take place in October 2012, the ceremony was cancelled at the very last minute due to what the organizers say ” was due to unforeseeable circumstances”.

The February 15 event will be held “under the theme ‘Rhythm Nation’ and promises to become one of the biggest awards events in Ghana”.

“We thank all the DJs, industry personnel, our fans and the press for bearing with us and supporting the movement through difficult times. It is our promise that things will be better in the coming years”, Chief Executive Officer of Merqury Republic says.

The Ghana DJ Awards is sponsored by Blue Jeans Energy Drink, Fiesta Condoms, Bensung Institute, Stallion Motors and Scratch Studios.

MAZEMBE TAYARI KWA KLABU BINGWA

Klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia Ya Kongo, imemuengia Nii Adgei kwenye kikosi chake kitakachoshiriki michuano ya klabu bingwa barani Afrika.

Nyota huyo wa zamani wa klabu ya Asante Kotoko imeenguliwa huku kukiwa na maswali mengi juu ya uamuzi huo wa klabu yake, lakini pia miamba hiyo ya Kongo na Barani Afrika, imetangaza kikosi chenye nyota 26 kitakachoshiriki michuano ya Afrika mwaka huu huku 3 wakitokea nchini Ghana ambao ni Yaw Farimpong,Richad Kisi Boateng,Gladson Awako na Solomon Asante.


kikosi kamili cha Mazembe mwaka huu kinaundwa na

Goal Keeper
1 Robert Muteba Kidiaba




21 Aime Bakula




22 Ley Matampi




Defender
2 Joel Kimwaki




3 Jean Kasusula




4 Eric Nkulukuta




5 Francis Kasonde




7 Herve Ndonga




16 Stophila Sunzu




17 Hichani Himonde




20 Pamphile Mihayo




33 Patient Mwepu




Midfielder
14 Nathan Sinkala




18 Rainford Kalaba




19 Tresor Salakiaku




23 Tresor Ilunga Kayanda




24 Narcisse Amia Ekanga




25 Patrick Ochan




26 Patrick Ilongo




27 Isaac Kasongo




29 Yannick Tusilu




30 Guy Lusadisu




32 Serge Lofo




Striker
6 Deo Kanda




8 Tresor Mputu




9 Cheibane Traore




10 Given Singuluma




11 Luka Lungu




15 Aly Mbwana Samata




28 Thomas Ulimwengu




31 Eric Bokanga




UNITED KUMSAJILI MGHANA

Klabu ya Manchester United imemchukua nyota wa Ghana na klabu ya Leicester City, Jeff Schlupp kwa majaribio wakiwa na lengo la kumsajili kwa mkataba wa kudumu endapo atafudhu majaribio hayo.

Schlupp, 20, ambaye hucheza nafasi ya ushambuliaji amekuwa kwenye mazoezi uwanja wa Carrington akiwa na ruhusa kutoka kwenye klabu yake, ambayo imekuwa na mahusiano ya karibu na United na mara kadhaa imekuwa ikichukua wachezaji kwa mkopo kutoka Manchester United.

Schlupp si mchezaji mwenye uzoefu hata kwenye ligi daraja la kwanza kwani mara ya mwisho kuchezea kikosi cha kwanza ilikuwa mwezi Novemba mwaka jana. Miongoni mwa vitu vilivyoivutia klabu hiyo ni uwezo wake wa kucheza kama mshambuliaji wa pembeni lakini pia kama beki wa kushoto kwenye klabu yake.

Zao hilo la kituo cha kukuza vipaji cha Leicester City kabla ya kuibuka msimu uliopita kwenye kikosi cha kwanza pia alicheza kwa mkopo klabu ya Brentford 2010-2011, huku akiifungia klabu yake mabao matatu (hat-trick) katika mchezo wake wa kwanza wa ligi daraja la kwanza akiwa na Leicetser dhidi ya Rotherham United katika kombe la ligi.

Mbali na kuwa uraia wa Ghana lakini ametumikia kikosi cha vijana cha Ujerumani, akiwa mzaliwa wa Hamburg kabla ya kuelekea nchini Uingereza akiwa bado mdogo kwa sasa ana mkataba na klabu yake unaombakisha hadi 2015.


Date of birth 23 December 1992 (age 20)
Place of birth Hamburg, Germany
Height 1.81 m (5 ft 11 12 in)
Playing position Forward / Left winger / Left back
Club information
Current club Leicester City
Number 18
Youth career
2005–2010 Leicester City
Senior career*
Years Team Apps (Gls)
2010– Leicester City 27 (2)
2011 Brentford (loan) 9 (6)
National team
2010 Germany U19

2011 Ghana 1 (0)

MWISHO WA KUCHUKUA FOMU TFF LEO