VIEW OTHER SITES
Wednesday
MAXIMO KUTUA BONGO KUIFUNDISHA YANGA
Kocha
wa zamani wa Taifa Stars, Mbrazili Marcio Maximo amewasili nchini ili kumalizia
mazungumzo yao ya kuingia mkataba na klabu ya Young Africans “Yanga”
kuifundisha kwa msimu ujao.
Yanga
ambao wameamua kukutana na kocha huyo baada ya kuondoka kwa aliyekuwa kocha wa
klabu hiyo, Mserbia Konstadin Papic ambaye aliondoka mwishoni mwa msimu
uliopita kuelekea kwao.
Maximo
alikuwa na Stars kutoka 2006 hadi 2010 mkataba wake ulipomalizika kabla ya
Mdenimaki Jan Poulsen kuchukua nafasi yake.
Mwaka
2009 aliiwezesha Tanzania kushiriki mashindano ya afrika wa wachezaji wa ndani
yaliyofanyika nchini Ivory Coast.
Yanga
ambayo inatarajiwa kufanya uchaguzi wake mnamo Juni 17 imemaliza nafasi ya 3
kwenye ligi kuu ya Vodadom msimu huu, inatarajiwa kushiriki mashindano ya
Afrika Mashariki na Kati baadaye mwaka huu pekee kwenye medani ya kimataifa
ikiingia kama bingwa mtetezi.
MILITO ATUNDIKA DARUGA
Beki
wa zamani wa Argentina, Gabriel Alejandro Milito ametangaza kustaafu soka
mwishoni mwa msimu huu baada ya kudumu kwa miaka 15 akiwa na vilabu tofauti barani Amerika ya
Kusini na Ulaya.
Milito
mwenye miaka 31 ambaye pia ni ndugu wa Mshambuliaji wa Inter Milan, Diego
Milito amechezea vilabu mbalimbali ikiwemo FC Barcelona, Real Zaragoza na sasa akiwa
na Independiente kama nahodha wa klabu hiyo.
Milito
ameanza soka lake na Independiente akiwa na mika 17 mwishoni mwa mwaka 1997
hadi 2003 alipohamia Zaragoza ya Uhispania akicheza kwa misimu minne ya
mafanikio kabla hajasaini na Barcelona 2007 ambapo aliachana nayo mwaka 2011.
Amepata
kuichezea timu yake ya taifa ya Argentina kwenye michezo 42 ikiwemo kombe la
dunia mwaka 2006 nchini Ujerumani.
Milito amezaliwa Septemba 7, 1980 jijini Bernal, Argentina.
MATAJI ALIYOTWAA;
Independiente
Argentine League: (1) Apertura 2002
Zaragoza
Kombe la Uhispania: (1) 2004
Barcelona
Ligi ya Uhispania(3): 2009, 2010, 2011
Kombe la Uhispania (1): 2009
Klabu bingwa Ulaya(2): 2009, 2011
Argentine League: (1) Apertura 2002
Zaragoza
Kombe la Uhispania: (1) 2004
Barcelona
Ligi ya Uhispania(3): 2009, 2010, 2011
Kombe la Uhispania (1): 2009
Klabu bingwa Ulaya(2): 2009, 2011
METODO; MFUMO WA KIITALIANO ULIOHAMISHIWA BARCELONA NA GUARDIOLA
Mfumo huu ulioasisiwa na kocha wa timu
ya taifa ya Italia, Vittorio Pozzo miaka ya 1930 ambapo mabeki wa kati
wanasaidia viungo huku mabeki wa pembeni wakiwa na jukumu kubwa la kusaidia
mashambulizi kutokea pembeni. Italia ilitumia mfumo huo kwenye kombe la dunia
1934 na 1938. Pia, Pep Guardiola alitumia mfumo huo akiwa na Barcelona ukiwa
umeboreshwa zaidi.
VITTORIO POZZO
KIKOSI CHA ITALIA MWAKA 1934 KIKIWA UWANJANI KABLA YA KUWAKABILI
JAMHURI YA CZECH KIKIONGOZWA NA NYOTA, Giuseppe De Meazza.
MWINYI MGENI RASMI TUZO ZA TASWA
RAIS mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya awamu ya pili, Alhaji Ally Hassan Mwinyi, amechaguliwa kuwa
mgeni rasmi katika sherehe za utoaji tuzo za wanamichezo bora Tanzania zitakazofanyika hapo kesho
kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama
cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Abbas Pinto amesema hayo
kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari mchana huu katika ukumbi wa City Sports
Lounge, jijini Dar es Salaam na kwamba wamemchangua Mwinyi kwa sababu alikuwa ana
mchango mkubwa katika sekta ya michezo enzi zake, akiwa Ikulu tangu 1985 hadi
1995 alipomuachia Benjamin William Mkapa.
Katika tuzo hizo,
kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Fadhil Hakizimana Niyonzima wa Yanga,
atachuana na Kipre Tchetche wa Ivory Coast anayechezea Azam FC na Mganda
Emmanuel Okwi wa Simba kuwania tuzo ya Mwanasoka Bora wa mwaka wa kigeni.
Kwa upande wa wanasoka
wazalendo, tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka inawaniwa na John Bocco, Aggrey
Morris, wote wa Azam na Juma Kaseja wa Simba, wakati kwa wachezaji wa Tanzania
wanaocheza nje wanaoshindana ni Henry Joseph wa Kongsvinger ya Norway na Mbwana
Samatta wa Tout Puissant Mazembe ya DRC.
Kwa upande wa
wanawake, Sophia Mwasikili anayecheza Uturuki, anashindana na Asha Rashid
‘Mwalala’, Mwanahamisi Omary wote wa Mburahati Queens, Fatuma Mustapha wa
Sayari na Eto’o Mlenzi wa JKT.
Tuzo hizo zinadhaminiwa
na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL).
Subscribe to:
Comments (Atom)



