Timu
za taifa za Czech na Ugiriki zimekuwa za kwanza kufika nchini Poland kwa
michuano ya Ulaya 2012 huku ikiwa zimebakia siku tano kabla ya kunza kwa
michuano hiyo mikubwa barani Ulaya.
Timu
zote zimepangwa kundi moja la A pamoja na Poland na Urusi, ambapo mechi za
kwanza zinatarajiwa kuchezwa ijumaa wiki hii kwa Poland kufungua dimba na
bingwa wa 2004,Ugiriki kwenye mji mkuu Warsaw huku Urusi akicheza na Jamhuri ya
Czech kusini magharibi mwa mji wa Wroclaw.
Jamhuri
ya Czech imewasili Wroclaw kutokea Prague kwa usafiri wa garimoshi lenye rangi
nyekundu, nyeupe na bluu zinazovaliwa na timu hiyo zikiwemo kwenye bendera ya
taifa lao, huku Ugiriki wakiwasili kwenye mji wa Warsaw.
Czech
wataingia uwanja wakiwa na nahodha wao, Thomas Roscicky aliyepata majeraha
madogo ambapo madaktari wa timu wamethibitisha kuwa atashiriki kwenye mchezo wa
kwanza dhidi ya Urusi huku akitarajiwa kukutana na nahodha wa Urusi na mchezaji
mwenzake wa zamani wa Arsenal, Andrey Arshavin.
Hata
hali ya usalama inaelekea kutiwa doa nchini humo kufuatia mpango wa kufanya
maandamano ulioandaliwa na kikundi cha watu wanaoipinga serikali mpya ya
Bronislaw Komorowski waliopanga kuandamana Juni, 10.

