VIEW OTHER SITES

Thursday


Rais wa Brazil Dilma Rousseff amesaini kuwa sheria muswada utakaoruhusu uuzwaji wa bia wakati wa mechi za Kombe la Dunia mwaka 2014.
Shirikisho la Soka Duniani, Fifa, lilikuwa likitaka kufanyiwa  mabadiliko katika sheria ya Brazil inayopiga marufuku pombe kuuzwa kwenye viwanja vya mpira wa miguu.
Muswada huo mpya umepitisha sheria kadhaa kwa ajili ya Kombe la Dunia, haujaelezea kuweka pingamizi lolote la kuuzwa pombe, uuzaji wa pombe ulikuwa mwiko katika mechi za kandanda nchini Brazil tangu mwaka 2003.
Upigwaji huo marufuku uliwekwa ikiwa ni sehemu ya hatua ya kupambana na vurugu miongoni mwa mashabiki wa timu zenye uhasama pamoja na kukabiliana na wahuni.
Mwanzoni mwa mwaka huu Katibu Mkuu wa Fifa, Jerome Valcke, aliweka bayana kwamba haki ya kuuza pombe ni lazima irejeshwe kuwa sheria wakati wa michuano ya Kombe la Dunia kwenye Bunge la Brazil.
Wakati wa ziara ya kukagua viwanja kwenye miji 12 ya Brazil itakayochezewa mechi hizo, alionesha hisia zake kwa jambo hilo.
"Unywaji wa pombe ni sehemu ya patashika za Kombe la Dunia, kwa hiyo tutahakikisha unaruhusiwa. Mtaniwia radhi iwapo nitakuwa nawakwaza kwa kiasi fulani lakini hilo ni jambo ambalo halina mjadala," alisema.
Kampuni ya bia ya Budweiser ndio wadhamini wakubwa wa Fifa.

RATIBA YA NBA LEO


Thu. 7 June

San Antonio Spurs@Oklahoma City Thunder
6:30 AM
SIX

Fri. 8 June

Miami Heat@Boston Celtics
6:00 AM
Ten Sports

VILLAREAL YAPOTEZA KOCHA NDANI YA SAA 24


Imebadilishwa:
Kocha wa klabu ya Real Madrid, Jose Mourinho ameongoza maelfu ya watu katika kutoa heshima zao kwa aliyekuwa kocha mpya aliyeteuliwa na klabu ya Villareal, Manuel Preciado ambaye amefariki saa 24 baada ya kutangazwa kuiongoza klabu hiyo nchini Uhispania.
Precado alikuwa kocha wa Sporting Gijon klabu ya mkataba huo alifariki kutokana na mshtuko wa moyo akiwa na umri wa miaka 54 huko jijini Valencia.
Kifo chake kimetokea saa 24 baada ya kusaini mkataba wa kuiongoza klabu ya Villareal iliyoshuka daraja, ambapo mkataba wake ulitarajiwa kuanza rasmi msimu wa mwaka 2012 hadi 2013.
Preciado alifukuzwa kazi na Sporting Gijon mnamo mwezi Januari licha ya kuiwezesha klabu hio kupanda daraja mara mbili kuingia Ligi kuu ya Uhispania, La Liga na kuifundisha kwenye mechi 232 kama kocha mkuu akiwa miongoni mwa makocha walioifundisha klabu hiyo kwa mafanikio zaidi nyuma ya Jose Manuel Diaz Novoa aliyeifundisha klabu kwenye mechi 282.
Enzi za uchezaji wake Preciado alicheza kama beki akianzia klabu ya Racing Santander kisha vilabu kama Linares, Mallorca, Alaves, Ourense na Gimnastica.
Mwaka 1992baada ya kustaafu soka aliaanza shughuli za ukufunzi akianzia klabu ya Gimnastica baadaye Racing B, Racing Santander, Levante na Murcia kabla ya kujiunga na Sporting Gijon mwaka 2006.