VIEW OTHER SITES

Sunday

KUYT KUTIMKIA UTURUKI

Klabu ya soka ya Liverpool maarufu kama majogoo wa jiji imeamua kumwachilia mshambuliaji wake raia wa Uholanzi, Dirk Kuyt(pichani) mwenye miaka 31 baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa misimu 6 akitokea Feyernoord ya Uholanzi.
Kuyt anatarajiwa kujiunga na Fernabahce ya Uturuki siku chache zijazo  kulingana na taarifa za mtandao wa klabu ya Liverpool, ambao hivi karibuni imemsajili kocha mpya, Brendan Rogders kutoka Swansea City.
Kuyt ambae anajiandaa na michuano ya Ulaya inayofanyika nchini Poland na Ukraine alijiunga na Liverpool 2006 akitokea Feyernoord ya Uholanzi akicheza mechi 285 na magoli 71 ikiwemo matatu (hat trick) dhidi ya Manchester United msimu ulipita.
Kuyt pia alifunga goli mojawapo kwenye mchezo wa fainali ya kombe la ligi mwezi Februari dhidi ya Cardiff City kwenye uwanja wa Wembley.

No comments:

Post a Comment