VIEW OTHER SITES

Sunday

MGOSI KUSAJILI JANGWANI


Mshambuliaji wa Daring Club Motema Pembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mussa Hassan Mgosi ametua nchini akitokea nchini Congo DR kutokana na kuendelea kwa mechi za kimataifa za kufuzu kucheza kombe la dunia 2014 zinazoendelea kwenye nchi mbalimbali barani Afrika.
Hata hivyo Mgosi anahusishwa na mipango ya kujiunga klabu ya Yanga ambayo ipo kwenye mchakato wa kupata viongozi wapya wa klabu hiyo kwa sasa.
Kwa upande wake Mgosi ambaye amepata kuzitumikia timu mbalimbali nchini zikiwemo Simba SC, Moro United akitokea shule ya sekondari ya Makongo amekana taarifa hizo kwa maelezo kuwa amekuja kutokana na matatizo ya kifamilia na atarejea DRC baada ya wiki mbili.

No comments:

Post a Comment