Mshambuliaji wa Daring Club Motema
Pembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mussa Hassan Mgosi ametua
nchini akitokea nchini Congo DR kutokana na kuendelea kwa mechi za kimataifa za
kufuzu kucheza kombe la dunia 2014 zinazoendelea kwenye nchi mbalimbali barani
Afrika.
Hata hivyo Mgosi anahusishwa na
mipango ya kujiunga klabu ya Yanga ambayo ipo kwenye mchakato wa kupata
viongozi wapya wa klabu hiyo kwa sasa.
Kwa upande wake Mgosi ambaye amepata
kuzitumikia timu mbalimbali nchini zikiwemo Simba SC, Moro United akitokea
shule ya sekondari ya Makongo amekana taarifa hizo kwa maelezo kuwa amekuja kutokana
na matatizo ya kifamilia na atarejea DRC baada ya wiki mbili.
No comments:
Post a Comment