Kisha wachezaji na viongozi wa Yanga wataelekea mkoani Dodoma kufuatia mwaliko wa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania na wapenzi wa klabu hiyo siku ya Jumatatu.
Mwaliko huo unatokana na kulitwaa
taji la klabu bingwa ya soka Afrika Mashariki na Kati,Kagame,
Jumamosi iliyopita, wakiifunga Azam FC mabao 2-0 kwenye fainali, Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam.
Julai 15, mwaka huu, Yanga ilipata uongozi mpya chini ya uenyekiti wa, Yussuf Manji, Makamu wake akiwa, Clement Sanga na wajumbe wanne wa kamati
ya utendaji, Abdallah Bin Kleb, George Manyama na Mussa Katabaro.
Wajumbe wengine waliosalia kutoka uongozi
uliopita, Mohamed Bhinda, Titto Osoro, Salim Rupia na Sarah Ramadhan
baada ya wajumbe wengine, wakiwemo Mwenyekiti, Wakili Lloyd Nchunga na Makamu
wake, Davis Mosha kujiuzulu.
No comments:
Post a Comment