Timu ya Coastal Union ya chini ya miaka 17 itamenyana na
Ecofoot ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC),kwenye mchezo wa fainali ya
mashindano ya Rollingston hapo kesho.
Coastal imetinga hatua hiyo baada ya kuwafunga mabingwa
watetezi wa michuano hiyo, Ruvu Shooting kwa mabao 2-1 nchini Burundi.
Mabao ya Coastal yakiwekwa kimiani na Mohamed Miraji, wakati
bao la Ruvu likifungwa naye, Said Hussein.
Timu ya Ecofoot imetinga hatua kufuatia ushindi wao dhidi ya
Mjini Magharibi ya Zanzibar wa mabao 2-1.
Mabao ya Ecofoot yalitiwa
kimiani na Sais Kabamba na Shukuru Hamisi, wakati bao la kufutia machozi la
Mjini Magharibi lilitiwa kimiani na Omar Tamim. Sasa, Mjini Magharibi
itamenyana na Ruvu katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu na Coastal
itamenyana na Ecofoot katika mechi ya kusaka bingwa mpya wa michuano hiyo
kesho.
No comments:
Post a Comment