Habari kutoka Simba SC zimesema kuwa, Okwi
amekwama na anarejea Simba SC, huku kukiwa na uvumi unaomhusisha mshambuliaji huyo wa zamani wa SC Villa ya Uganda na kuelekea mtaa wa Jangwani ikiwa ni mipango ya uongozi mpya wa Yanga kuimarisha safu ya ushambuliaji.
Kwa sasa Okwi yuko nchini Uganda kutoka
Austria, kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa wa Malaria.
Hata hivyo Katibu wa Simba Evodius Mtawala amesema kuwa; “Okwi amefuzu majaribio, ila ana Malaria, amekuja
kuitibu kisha atarudi Austria kwa ajili ya vipimo,”alisema Mtawala.
Klabu hiyo ya Austria ilipanga kuipa Simba SC Euro 600,000,
Hapo kabla, Simba ilipata ofa ya Sh. Bilioni 2 kutoka kwa miamba ya soka ya Afrika Kusini,
Mamelodi Sundown lakini mshambuliaji huyo hakuwa tayari kujiunga na klabu hiyo.
Lakini pia, Olando Pirates ya Afrika Kusini ilimuomba Okwi
akafanye majaribio huko kama angefuzu wangemsajili dau la dola 550,000 kabla ya
kuibuka kwa taarifa za kutakiwa na klabu ya Parma ya Italia.
No comments:
Post a Comment