VIEW OTHER SITES

Monday

MANJI ATINGA JANGWANI KUCHUKUA FOMU


Mdhamini wa klabu ya soka ya Yanga, YUSSUF Mehboob Manji, ametinga makao makuu ya klabu hiyo na kuchukua fomu za kugombea nafasi ya uongozi klabuni humo, klabu hiyo iliyopo kwenye makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani leo mashabiki waliduwaa baada bosi huyo wa klabu ya Yanga kutinga kwenye ofisi za klabu hiyo hii leo.
Hata hivyo imetaarifiwa kuwa Manji amewachukulia fomu za kugombea uongozi, wanachama watatu, katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Julai 15, mwaka huu mjini Dar es Salaam mbali na yeye kuhusishwa na kutaka kugombea nafasi ya uenyekiti klabuni hapo.
Katibu Mkuu wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Francis Kaswahili amesema kwamba Manji amewachukulia fomu wanachama watatu, ambao ni Abdallah Bin Kleb na Muhingo Rweyemamu kwa ajili ya nafasi za Ujumbe wa Kamati ya Utendaji na Isaac Chanji kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti.
Lakini bado kuna uvumi kwamba Manji mwenyewe wakati wowote atachukua fomu ya kuwania Uenyekiti, ingawa awali ilielezwa anamuunga mkono Francis Kifukwe awanie nafasi hiyo.
Kuchukua fomu kwa wajumbe hao watatu, kunafanya idadi ya waliochukua fomu hadi sasa kufika 10, baada ya awali Ayoub Nyenzi kuchukua fomu ya kugombea Makamu Mwenyekiti, Jumanne Mwamenywa, John Jambele, Peter Haule,
Gaudicius Ishengoma, Abdallah Sharia na Saleh Abdallah, wote Ujumbe.

No comments:

Post a Comment