Mabao
mawili ya Javier Hernandez “Chicharito” na Giovani Dos Santos yameiwezesha
Mexico kupata ushindi wa 2-0 dhidi ya Brazil kwenye mchezo wa kimataifa wa
kirafiki.
Goli
la kwanza la Mexico lilifungwa dakika ya 21 kupitia kwa Dos Santos kabla ya
Chicharito kufunga goli la pili dakika ya 32 kwa njia ya mkwaju wa penati.
Mchezo
huo uliopigwa uwanja wa Cowboys wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 84 519
ulikuwa wa kujipima nguvu kwa Brazil inayoshiriki mashindano ya Olimpiki mwezi
Julai nchini Uingereza, huku Mexico ikijiandaa na mchezo wao na Guyana ili
kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kombe la dunia nchini Brazil 2014.

No comments:
Post a Comment