VIEW OTHER SITES

Monday

KIEMBA, SHAMTE WAREJEA MSIMBAZI


Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Simba SC, Ibrahim Masoud ‘Maestro’ ametangaza kurejea kwa kiungo, Amiri Kiemba na Haruna Shamte leo mchana.
Kiemba aliyekataa kwenda kujiunga na Polisi Dodoma kwa kutokufikia makubaliano, wakati Shamte aliichezea Villa Squad iliyoshuka daraja.
Maestro akizungumza mchana huu amesema kwamba baada ya wachezaji hao kumaliza muda wao wa kuwa nje kwa mkopo, klabu itaangalia kama itawatoa tena kwa mkopo au itawarejesha kikosini.
Lakini habari za ndani zinadai kwamba wachezaji hao watarejeshwa kikosini, kwa sababu ya umuhimu wao na badala yake, beki Victor Costa na kiungo Salum Machaku ndio watatolewa kwa mkopo.  
Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Simba SC, Ibrahim Masoud ‘Maestro’ amesema kwamba, Kiemba alikataa kabisa kwenda kuichezea Polisi Dodoma kwa sababu hawakufikia makubaliano, wakati Shamte aliichezea Villa Squad iliyoshuka daraja.
Baada ya wachezaji hao kumaliza muda wao wa kuwa nje kwa mkopo, klabu itaangalia kama itawatoa tena kwa mkopo au itawarejesha kikosini.

No comments:

Post a Comment