Mwenyekiti wa Kamati
ya Ufundi ya Simba SC, Ibrahim Masoud ‘Maestro’ ametangaza kurejea kwa kiungo,
Amiri Kiemba na Haruna Shamte leo mchana.
Kiemba aliyekataa kwenda
kujiunga na Polisi Dodoma kwa kutokufikia makubaliano, wakati Shamte aliichezea
Villa Squad iliyoshuka daraja.
Maestro akizungumza mchana
huu amesema kwamba baada ya wachezaji hao kumaliza muda wao wa kuwa nje kwa
mkopo, klabu itaangalia kama itawatoa tena kwa mkopo au itawarejesha kikosini.
Lakini habari za ndani
zinadai kwamba wachezaji hao watarejeshwa kikosini, kwa sababu ya umuhimu wao
na badala yake, beki Victor Costa na kiungo Salum Machaku ndio watatolewa kwa
mkopo.
Mwenyekiti wa Kamati
ya Ufundi ya Simba SC, Ibrahim Masoud ‘Maestro’ amesema kwamba, Kiemba alikataa
kabisa kwenda kuichezea Polisi Dodoma kwa sababu hawakufikia makubaliano,
wakati Shamte aliichezea Villa Squad iliyoshuka daraja.
Baada ya wachezaji hao
kumaliza muda wao wa kuwa nje kwa mkopo, klabu itaangalia kama itawatoa tena
kwa mkopo au itawarejesha kikosini.

No comments:
Post a Comment