VIEW OTHER SITES

Friday

Twiga stars yawasili Ethhiopia bila Mwasikili


Kikosi cha timu ya taifa ya wanawake nchini, Twiga Stars kimefika salama nchi Ethiopia tayari kuikabili timu hiyo kwenye mchezo wa mchujo ili kupata nafasi ya kushiriki kombe la mataifa ya Afrika 2012 yatayofanyika nchini Guinea ya Ikweta.
Kikosi kilicho chini ya kocha mzawa, Charles Boniface Mkwasa imefikia hoteli ya Churchill jijini Addis Ababa baada ya kuwasili saa moja na nusu sawa na saa mbili na nusu usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Mchezo huo utapigwa tarehe 27 mwezi huu kwenye uwanja wa Addis Ababa, awapo awali Twiga Stars waliitoa timu ya taifa ya Namibia kwa jumla ya magoli 7-2.
Hata hivyo Twiga stars watamkosa beki Sofia Mwasikili ambaye klabu yake ya nchini uturuki haijamwachilia kwa mcezo huo utakaopigwa jumapili hii.

No comments:

Post a Comment