Kikosi cha timu ya taifa ya wanawake nchini, Twiga Stars kimefika
salama nchi Ethiopia tayari kuikabili timu hiyo kwenye mchezo wa mchujo ili
kupata nafasi ya kushiriki kombe la mataifa ya Afrika 2012 yatayofanyika nchini
Guinea ya Ikweta.
Kikosi kilicho chini ya kocha mzawa, Charles Boniface Mkwasa imefikia
hoteli ya Churchill jijini Addis Ababa baada ya kuwasili saa moja na nusu sawa
na saa mbili na nusu usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Mchezo huo utapigwa tarehe 27 mwezi huu kwenye uwanja wa Addis Ababa,
awapo awali Twiga Stars waliitoa timu ya taifa ya Namibia kwa jumla ya magoli
7-2.
Hata hivyo Twiga stars watamkosa beki Sofia Mwasikili ambaye klabu
yake ya nchini uturuki haijamwachilia kwa mcezo huo utakaopigwa jumapili hii.
No comments:
Post a Comment