VIEW OTHER SITES

Friday

BOLT ASHINDWA KUVUNJA REKODI YAKE CZECH



Mwanariadha mjamaica, Usain Bolt hii leo amefanikiwa kushinda mbio za mitaa 100 zilizofanyika Golden Spike, Ostrava,Jamhuri ya Czech.
Katika mbio hizo kuelekea mashindano makubwa ya olimpiki jijini London yalishuhudiwa kwa Bolt kushiriki kwa mara ya sita katika mbio zilizofanyika kwenye mji huo ambapo alishinda kwa sekunde 10.04.
Ushindi huo ni wa kwanza kwa Bolt kwenye ardhi ya Ulaya kuelekea mashindano ya Olimpiki, kwa upande mwingine nafasi ya pili ilienda kwa Kim Collins raia wa visiwa vya St. Kitts na Nevis aliyetumia sekunde 10.19, akifuatiwa na Darvis Patton wa Marekani aliyetumia sekunde 10.22.
Hata hivyo Bolt alishindwa kuvunja rekodi yake ya sekunde 9.82 aliyoiweka mwanzoni mwa mwezi Mei nchini Jamaica.
Bolt ni mshindi wa medali tatu za dhahabu kwenye mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika 2008 Beijing, Japan.

No comments:

Post a Comment