VIEW OTHER SITES

Friday

MAANDALIZI YA UMISSETA MWANZA YASHIKA KASI


Maandalizi ya mashindano ya UMISSETA mwaka huu kwa ngazi ya mkoa wa Mwanza yazidi kupamba moto kwenye shule ya sekondari Nsumba ambapo ni kituo cha mashindano hayo kwa mkoa wa Mwanza.
Mashindano hayo yanatarajiwa kufungua pazia lake mnamo Juni,2 kwa kushirikisha wilaya zote za mkoa wa Mwanza, miongoni mwa michezo itakayohusika ni pamoja na soka, pete, kikapu, wavu, riadha, tenisi, mikono na bao.
Akizungumzia mashindano hayo, mratibu wa UMISSETA kanda, Kabuche Suleiman Enock Shaibu amesema kuwa, maandalizi ya mashindano ya mwaka huu yako vizuri na wanatarajia upinzani baina ya wilaya zitakazoshiriki mashindano ya mwaka huu kutokana na maandalizi yao.
Lakini pia ameelezea changamoto wanazokutana nazo ikiwemo vifaa vya mchezo ikiwemo mipira huku akitoa amasa kwa wadau wa michezo kijitokeza kuwezesha mashindano hayo yafanyike kwa ustadi zaidi, hata hivyo UMISSETA kwa sasa jiji ndilo linajitoa zaidi kusaidia mashindano hayo.
Wilaya zitakazoshiriki mashindano ya mwaka huu ni Nyamagana, Ilemela, Magu, Misungwi, Kwimba, Sengerema, Ukerewe na Geita.

No comments:

Post a Comment