Maandalizi ya mashindano ya UMISSETA mwaka huu kwa ngazi ya mkoa wa
Mwanza yazidi kupamba moto kwenye shule ya sekondari Nsumba ambapo ni kituo cha
mashindano hayo kwa mkoa wa Mwanza.
Mashindano hayo yanatarajiwa kufungua pazia lake mnamo Juni,2 kwa kushirikisha
wilaya zote za mkoa wa Mwanza, miongoni mwa michezo itakayohusika ni pamoja na
soka, pete, kikapu, wavu, riadha, tenisi, mikono na bao.
Akizungumzia mashindano hayo, mratibu wa UMISSETA kanda, Kabuche
Suleiman Enock Shaibu amesema kuwa, maandalizi ya mashindano ya mwaka huu yako
vizuri na wanatarajia upinzani baina ya wilaya zitakazoshiriki mashindano ya
mwaka huu kutokana na maandalizi yao.
Lakini pia ameelezea changamoto wanazokutana nazo ikiwemo vifaa vya
mchezo ikiwemo mipira huku akitoa amasa kwa wadau wa michezo kijitokeza
kuwezesha mashindano hayo yafanyike kwa ustadi zaidi, hata hivyo UMISSETA kwa
sasa jiji ndilo linajitoa zaidi kusaidia mashindano hayo.
Wilaya zitakazoshiriki mashindano ya mwaka huu ni Nyamagana, Ilemela,
Magu, Misungwi, Kwimba, Sengerema, Ukerewe na Geita.
No comments:
Post a Comment