VIEW OTHER SITES

Friday

GUARDIOLA KUFUNGA KAZI NA BARCELONA LEO


Klabu ya FC Barcelona wataikabili Athletic Bilbao hii leo kwenye mchezo wa fainali ya kombe la mfalme nchini uhispania utakaopigwa umanja wa Vicente Calderon jijini Madrid.
Kocha Pep Guardiola atakalia benchi la ufundi la klabu hiyo kwa mara ya mwisho kuiongoza Barcelona kwenye mchezo huo wa fainali ya 7 dhidi ya Bilbao.
Barcelona imetwaa mataji 25 ya kombe la mfalme akifuatiwa na Bilbao iliyotwaa mara 23, kati ya mara 6 ilizokutana Barcelona wameshinda mara 4 huku Bilbao wakishinda mara 2.
Fainali hii itampatia taji la 14 Guardiola endapo Barcelona watashinda dhidi ya Bilbao iliyocheza kwa mara ya mwisho 1984.
Barcelona wataingia uwanjani bila ya Puyol, Abidal na beki wa kulia, Dani Alves atakayekuwa nje kwa majuma sita hadi nane baada ya kuumia mguu wa kulia akiwa mazoezini huku Bilbao walio chini ya Muargentina, Marcelo Bielsa wataingia wakiwa na mshambuliaji wao wa kutumainiwa, Fernando Llorente Torres mwenye magoli matano kwenye ligi hiyo. Vikosi vitakavyochuana hii leo,
BILBAO:Iraizoz;Iraola, Martinez, Amorebieta, Aurtenetxe;
De Marcos, Iturraspe, Herrera;Susaeta, Llorente, Muniain
BARCELONA:Pinto;Montoya, Pique, Mascherano, Adriano;Xavi, Busquets, Iniesta;Fabregas, Messi, Alexis.

No comments:

Post a Comment