Klabu ya FC Barcelona wataikabili Athletic Bilbao hii leo kwenye
mchezo wa fainali ya kombe la mfalme nchini uhispania utakaopigwa umanja wa
Vicente Calderon jijini Madrid.
Kocha Pep Guardiola atakalia benchi la ufundi la klabu hiyo kwa mara
ya mwisho kuiongoza Barcelona kwenye mchezo huo wa fainali ya 7 dhidi ya Bilbao.
Barcelona imetwaa mataji 25 ya kombe la mfalme akifuatiwa na Bilbao
iliyotwaa mara 23, kati ya mara 6 ilizokutana Barcelona wameshinda mara 4 huku
Bilbao wakishinda mara 2.
Fainali hii itampatia taji la 14 Guardiola endapo Barcelona watashinda
dhidi ya Bilbao iliyocheza kwa mara ya mwisho 1984.
Barcelona wataingia uwanjani bila ya Puyol, Abidal na beki wa kulia,
Dani Alves atakayekuwa nje kwa majuma sita hadi nane baada ya kuumia mguu wa
kulia akiwa mazoezini huku Bilbao walio chini ya Muargentina, Marcelo Bielsa
wataingia wakiwa na mshambuliaji wao wa kutumainiwa, Fernando Llorente Torres
mwenye magoli matano kwenye ligi hiyo. Vikosi vitakavyochuana hii leo,
BILBAO:Iraizoz;Iraola,
Martinez, Amorebieta, Aurtenetxe;
De Marcos, Iturraspe, Herrera;Susaeta, Llorente, Muniain
BARCELONA:Pinto;Montoya,
Pique, Mascherano, Adriano;Xavi, Busquets, Iniesta;Fabregas, Messi, Alexis.
No comments:
Post a Comment