MSHAMBULIAJI wa Simba SC na raia wa Uganda, Emmanuel Arnold
Okwi anaweza kuuzwa na klabu yake kwa moja ya klabu za nchini Austria kwa
gharama ya dola za Kimarekani 500,000 (sawa
na Sh. Milioni 750 za Tanzania) na kuweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyewahi
kuuzwa kwa bei ghali zaidi ndani ya klabu ya Simba SC.
Rekodi hiyo inashikiliwa na Mbwana Ally Samatta aliyeuzwa kwa
dola za Kimarekani 100,000 kwenda klabu ya Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo (DRC) msimu uliopita.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya klabu ya Simba, ambazo
blog hii imezipata zinasema kwamba, Okwi mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda,
mwenye umri wa miaka 19 aliyetua Msimbazi msimu wa 2010 akitokea klabu ya SC Villa ya Uganda anatakiwa
na klabu hiyo kwa dau hilo.
Ofa hiyo tayari iko mezani kwa Simba na kwa sasa inafanyiwa
kazi kabla ya wakati wowote kutangazwa rasmi kuuzwa kwa mchezaji huyo,
aliyesajiliwa na Wekundu wa Msimbazi, kwa dau la dola za Kimarekani 5000.
No comments:
Post a Comment