VIEW OTHER SITES

Friday

OKWI ATAKIWA AUSTRIA


MSHAMBULIAJI wa Simba SC na raia wa Uganda, Emmanuel Arnold Okwi anaweza kuuzwa na klabu yake kwa moja ya klabu za nchini Austria kwa gharama ya dola za Kimarekani 500,000    (sawa na Sh. Milioni 750 za Tanzania) na kuweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyewahi kuuzwa kwa bei ghali zaidi ndani ya klabu ya Simba SC.

Rekodi hiyo inashikiliwa na Mbwana Ally Samatta aliyeuzwa kwa dola za Kimarekani 100,000 kwenda klabu ya Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) msimu uliopita.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya klabu ya Simba, ambazo blog hii imezipata zinasema kwamba, Okwi mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, mwenye umri wa miaka 19 aliyetua Msimbazi msimu wa 2010 akitokea klabu ya SC Villa ya Uganda anatakiwa na klabu hiyo kwa dau hilo.

Ofa hiyo tayari iko mezani kwa Simba na kwa sasa inafanyiwa kazi kabla ya wakati wowote kutangazwa rasmi kuuzwa kwa mchezaji huyo, aliyesajiliwa na Wekundu wa Msimbazi, kwa dau la dola za Kimarekani 5000.

No comments:

Post a Comment