VIEW OTHER SITES

Friday

UNITED KUMSAJILI MGHANA

Klabu ya Manchester United imemchukua nyota wa Ghana na klabu ya Leicester City, Jeff Schlupp kwa majaribio wakiwa na lengo la kumsajili kwa mkataba wa kudumu endapo atafudhu majaribio hayo.

Schlupp, 20, ambaye hucheza nafasi ya ushambuliaji amekuwa kwenye mazoezi uwanja wa Carrington akiwa na ruhusa kutoka kwenye klabu yake, ambayo imekuwa na mahusiano ya karibu na United na mara kadhaa imekuwa ikichukua wachezaji kwa mkopo kutoka Manchester United.

Schlupp si mchezaji mwenye uzoefu hata kwenye ligi daraja la kwanza kwani mara ya mwisho kuchezea kikosi cha kwanza ilikuwa mwezi Novemba mwaka jana. Miongoni mwa vitu vilivyoivutia klabu hiyo ni uwezo wake wa kucheza kama mshambuliaji wa pembeni lakini pia kama beki wa kushoto kwenye klabu yake.

Zao hilo la kituo cha kukuza vipaji cha Leicester City kabla ya kuibuka msimu uliopita kwenye kikosi cha kwanza pia alicheza kwa mkopo klabu ya Brentford 2010-2011, huku akiifungia klabu yake mabao matatu (hat-trick) katika mchezo wake wa kwanza wa ligi daraja la kwanza akiwa na Leicetser dhidi ya Rotherham United katika kombe la ligi.

Mbali na kuwa uraia wa Ghana lakini ametumikia kikosi cha vijana cha Ujerumani, akiwa mzaliwa wa Hamburg kabla ya kuelekea nchini Uingereza akiwa bado mdogo kwa sasa ana mkataba na klabu yake unaombakisha hadi 2015.


Date of birth 23 December 1992 (age 20)
Place of birth Hamburg, Germany
Height 1.81 m (5 ft 11 12 in)
Playing position Forward / Left winger / Left back
Club information
Current club Leicester City
Number 18
Youth career
2005–2010 Leicester City
Senior career*
Years Team Apps (Gls)
2010– Leicester City 27 (2)
2011 Brentford (loan) 9 (6)
National team
2010 Germany U19

2011 Ghana 1 (0)

No comments:

Post a Comment