VIEW OTHER SITES

Wednesday

MAXIMO KUTUA BONGO KUIFUNDISHA YANGA


Kocha wa zamani wa Taifa Stars, Mbrazili Marcio Maximo amewasili nchini ili kumalizia mazungumzo yao ya kuingia mkataba na klabu ya Young Africans “Yanga” kuifundisha kwa msimu ujao.
Yanga ambao wameamua kukutana na kocha huyo baada ya kuondoka kwa aliyekuwa kocha wa klabu hiyo, Mserbia Konstadin Papic ambaye aliondoka mwishoni mwa msimu uliopita kuelekea kwao.
Maximo alikuwa na Stars kutoka 2006 hadi 2010 mkataba wake ulipomalizika kabla ya Mdenimaki Jan Poulsen kuchukua nafasi yake.
Mwaka 2009 aliiwezesha Tanzania kushiriki mashindano ya afrika wa wachezaji wa ndani yaliyofanyika nchini Ivory Coast.
Yanga ambayo inatarajiwa kufanya uchaguzi wake mnamo Juni 17 imemaliza nafasi ya 3 kwenye ligi kuu ya Vodadom msimu huu, inatarajiwa kushiriki mashindano ya Afrika Mashariki na Kati baadaye mwaka huu pekee kwenye medani ya kimataifa ikiingia kama bingwa mtetezi.

No comments:

Post a Comment