VIEW OTHER SITES

Wednesday

MILITO ATUNDIKA DARUGA


Beki wa zamani wa Argentina, Gabriel Alejandro Milito ametangaza kustaafu soka mwishoni mwa msimu huu baada ya kudumu kwa miaka 15  akiwa na vilabu tofauti barani Amerika ya Kusini na Ulaya.
Milito mwenye miaka 31 ambaye pia ni ndugu wa Mshambuliaji wa Inter Milan, Diego Milito amechezea vilabu mbalimbali ikiwemo FC Barcelona, Real Zaragoza na sasa akiwa na Independiente kama nahodha wa klabu hiyo.
Milito ameanza soka lake na Independiente akiwa na mika 17 mwishoni mwa mwaka 1997 hadi 2003 alipohamia Zaragoza ya Uhispania akicheza kwa misimu minne ya mafanikio kabla hajasaini na Barcelona 2007 ambapo aliachana nayo mwaka 2011.
Amepata kuichezea timu yake ya taifa ya Argentina kwenye michezo 42 ikiwemo kombe la dunia mwaka 2006 nchini Ujerumani.
Milito amezaliwa Septemba 7, 1980 jijini Bernal, Argentina.
MATAJI ALIYOTWAA;
Independiente 
Argentine League: (1) Apertura 2002

Zaragoza
Kombe la Uhispania: (1) 2004

Barcelona
Ligi ya Uhispania(3): 2009, 2010, 2011
Kombe la Uhispania (1): 2009
Klabu bingwa Ulaya(2): 2009, 2011

No comments:

Post a Comment