Tiketi za mechi ya
pili ya kufuzu kombe la dunia 2014 nchini Brazil kati ya Tanzania “Taifa Stars”
na Gambia “Nge” zinaanza kuuzwa leo kuanzia majira ya saa 2 asubuhi kwenye
vituo vya Mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora na Ohio, Shule ya Sekondari
Benjamin Mkapa, Soko Kuu la Kariakoo na Uwanja wa Taifa.
Ofisa Habari wa
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura Mgoyo amesema kuwa mauzo
yataendelea hadi siku ya mechi kwenye vituo husika kati ya saa 2 asubuhi hadi
saa 6 mchana kisha kuhamia Uwanja wa Taifa.
Viingilio vya mechi
hiyo vitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani ambavyo ni 36,693
kati ya jumla ya viti 57,558 vilivyopo katika uwanja huo wa kisasa sawa na
asilimia 63.7 ya watu watakaoshuhudia mchezo, viti vya rangi ya chungwa ni sh.
5,000, huku kwa upande wa VIP C watatozwa sh. 10,000 na VIP B itakuwa sh.
20,000. Kwa upande wa jukwaa la VIP A ambalo linachukua watazamaji 748 tu ambao
ni asilimia 1.3 ya watu wote watalipia sh. 30,000.
Mechi hiyo itachezwa
Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itaanza majira ya saa 10 kamili
jioni.
Msafara wa timu hiyo
wenye watu 31 wakiwemo wachezaji 22 unaongozwa na
Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Vijana na Michezo wa Gambia, Malang Jassey.
Viongozi wengine ni
Ofisa Utawala wa timu, Modou Sowe, Kocha Luciano Mancini, makocha wasaidizi,
Peter Bonu Johnson na Lamin Sambou, Kocha wa makipa Alhagie Marong, mtaalamu wa
tiba ya mifupa, Pa Matarr Ndow, mtunza vifaa, Sanna Bojang na daktari wa timu,
Kalifa Manneh.
Wachezaji waliopo ni
Musa Camara, Abdou Jammeh, Momodou Futty Danso, Lamin Basmen Samateh, Ousman
Koli, Pa Saikou Kujabi, Mustapha Kebba Jarju, Yankuba Mal Ceesay, Demba Savage,
Saihou Gassama, Alieu Darboe, Momodou Ceesay, Pa Modou Jagne, Tijan Jaiteh,
Bubacarr Sanyang, Christopher Allen, Musa Yaffa, Sulayman Marr, Mamut Saine,
Hamsa Barry, Ali Sowe, Omar Colley na Saloum Faal.
Saa 4 kamili asubuhi ya
leo kutakuwa na mkutano kati ya makocha wa timu zote mbili Kim Poulsen wa Taifa
Stars na Luciano Mancini wa The Scorpions wakiwa na manahodha wao, Juma Kaseja “Taifa
Stars” na Mustapha Jarju"Toubabo" mbele ya waandishi wa Habari utakaofanyika ofisi za Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF).

No comments:
Post a Comment