VIEW OTHER SITES

Saturday

TEGETE WA YANGA HADI 2014


Klabu ya soka ya YANGA imefanikiwa kumbakisha mshambuliaji wake,  Jerryson Tegete ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili ya kuichezea Yanga hadi 2014.
Jerry amesema kwamba amesaini mkataba wa miaka miwili zaidi kuendelea kuichezea Yanga.          “Nimesaini leo, mimi ni mchezaji halali wa Yanga, kweli kabla ya kusaini na hali ya mambo ilivyokuwa Yanga niliwahi kufanya mazungumzo na viongozi wa Simba na Azam, ilikuwa tunaelekea kukubaliana, ila sasa nashukuru hali imetulia klabuni, nami nimesaini leo,”alisema Tegete.  
Habari zisizo na shaka kutoka mitaa ya Twiga na Jangwani zinasema kwamba Tegete ambaye amemaliza mkataba wake mwezi huu, amesaini kwa watu ambao wamepewa kazi ya kufanya zoezi la usajili, Abdallah Ahmad Bin Kleb na Seif Ahmad ‘Magari’.
Simba imeshindwa kuwabakisha kipa wao, Ally Mustafa Mtinge ‘Barthez’ na beki wa kati Kelvin Patrick Yondan “Vidic” ambao wamekubali kusaini Yanga.
Jerry alitua Yanga mwaka 2008, akitokea sekondari ya Makongo na kujihakikishia namba kwenye timu hiyo kwa kupachika mabao hususani katika mechi zilizowakutanisha watani wa jadi.

Kwa upande wao Simba wamemsajili Kigi Makasi kutoka kwa mahasimu wao.

No comments:

Post a Comment