Bodi ya Taifa ya
Mashindano ya Miss Utalii Tanzania imegawa mikoa yote ya Tanzania na Vyuo
Vikuu katika kanda maalumu za mashindano hayo.
Kuanzia mwaka huu
kutakuwa na kanda 14, zikiwemo
saba (7) za kawaida na saba (7) kanda maalumu za Miss Utalii vyuo Vikuu.
Hatua hiyo imelenga kufikisha
mashindano hayo katika ngazi za chini zaidi ambapo kwa
kuanzia mashindano haya yataanzia katika ngazi za kata, majimbo ,wilaya,mikoa,
kanda, taifa na hatimaye dunia, huku mpango mkakati ni kuanza kufanyika katika
mgazi za vijiji ifikapo mwaka 2014.
Mgawanyo wa kanda hizo na
mikoa yake katika mabano ni:
A: KANDA ZA KAWAIDA NI:
1. Miss Utalii Tanzania
–Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Lindi na Mtwara, Zanzibar)
2. Miss Utalii Tanzania –
Kanda ya Magharibi (Simiyu, Shinyanga na Mara)
3. Miss Utalii Tanzania –
Kanda ya Ziwa (Mwanza, Geita, Kagera na Kigoma)
4. Miss Utalii Tanzania –
Kanda ya Kaskazini (Arusha, Kilimanjaro na Arusha)
5. Miss Utalii Tanzania –
Kanda ya Kati (Tabora, Dodoma, Singida na Morogoro)
6. Miss Utalii Tanzania –
Kanda ya Kusini Nyanda za Juu (Mbeya, Rukwa na Katavi)
7. Miss Utalii Tanzania –
Kanda ya Kusini (Ruvuma, Iringa na Njombe)
B: KANDA MAALUM ZA VYUO
VIKUU NI:
1. Miss Utalii Tanzania
Vyuo Vikuu – Kanda ya Kati (Dodoma, Kigoma, Tabora, Singida)
2. Miss Utalii Tanzania
Vyuo Vikuu – Kanda ya Kusini (Iringa, Ruvuma, Njombe)
3. Miss Utalii Tanzania
Vyuo Vikuu – Kanda ya Pwani (Dar es Salaam, Zanzibar , Lindi na Mtwara)
4. Miss Utalii Tanzania
Vyuo Vikuu- Kanda ya Magharibi (Mwanza, Geita, Kagera, Mara, Simiyu, Shinyanga
na Singida)
5. Miss Utalii Tanzania
Vyuo Vikuu – Kanda ya Kusini Nyanda za Juu (Mbeya, Rukwa, Katavi)
6. Miss Utalii Tanzania
Vyuo Vikuu – Kanda ya Kaskazini ( Arusha,Kilimanjaro,Manyara)
7. Miss Utalii Tanzania
Vyuo Vikuu – Kanda ya Mashariki (Morogoro, Mtwara na Lindi)
Mgawanyo huu wa kanda
umezingatia , maeneo ya kijografia, mwingiliano wa tamaduni, uwepo wa vivutio
vya Utalii katika kila kanda, urahisi wa kutangaza Utalii na kuhamasisha Utalii
wa ndani,pia kutoa fulsa kwa mabinti wengi zaidi kushiriki mashindano haya
katika Ngazi zote.
Kwa mwaka huu, kanda ya
ziwa ndiyo itakayo kuwa ya kwanza kufanya Fainali zake za Miss Utalii Kanda ya
Ziwa 2012 na kushirikisha jumla ya warembo 15 kutoka mikoa ya Mwanza, Kagera,
Geita na Kigoma.
Shindano hilo limepangwa
kufanyika Juni 30, 2012 katika ukumbi wa Monarch Hotel Mwanza.

No comments:
Post a Comment