VIEW OTHER SITES

Thursday

BAYERN YAMNASA GUARDIOLA

Klabu ya Bayern Munich ya nchini Ujerumani imemtangaza kocha wa zamani wa FCBarcelona, Josep Guardiola kuchukua pahali pa kocha wa sasa wa klabu hiyo, Jupp Heynckes mwishoni mwa msimu huu.

 Guardiola, mwenye  miaka 41, atachukua nafasi ya Heynckes, aliyekataa kuongeza mkataba na mimba hiyo ya Ujerumani na barani Ulaya mwezi Julai. 

"Tumefurahi kufanikiwa kumshawishi mtu mwenye uwezo kama Pep Guardiola, ambaye amekuwa akitakiwa na vilabu mbalimbali vikubwa barani Ulaya, kujiunga na Bayern Munich," alisema mkurugenzi mkuu wa Bayern,Karl-Heinz Rummenigge hapo jana.

"Pep Guardiola ni miongoni mwa makocha wenye mafanikio ya juu kabisa duniani na natumaini ataleta tija kubwa kwa klabu yetu na soka la Ujerumani. aliongeza Rummenigge 

Guardiola aliachana na miamba ya Uhispania kutoka jimbo la Katalunya, FC Barcelona msimu uliopita baada ya kuiongoza klabu hiyo kutwaa mataji 14 ndani ya misimu minne ikiwemo 2 klabu bingwa barani Ulaya, 3 ligi kuu nchini Uhispania na 1 klabu bingwa ya dunia.

 Bayern kwa sasa inaongoza ligi kuu ya Ujerumani maarufu kama Bundesliga ikiwa alama tisa mbele ya Bayer 04 Leverkusen ikiwa na alama 42 baada ya michezo 17 ya ligi hiyo.

Miongoni mwa matarajio ya wengi ni kuona TRINITY  ya Barcelona baina ya Xavi, Iniesta na Messi ikihamia klabuni hapo huku Toni Kroos, Xherdan Shaqiri, na Bastian Schweinsteiger wakipewa nafasi kubwa ya kuwa chaguo la kocha huyo mpya.

Ligi hiyo intarajiwa kuendelea tena hapo kesho Ijumaa kwa Shalke 04 kuivaa Hannover 96, huku mechi zingine zikipigwa Jumamosi

19 Jan, 14:30 FSV Mainz 05 v SC Freiburg
Coface Arena, Mainz
19 Jan, 14:30 Bayern Munich v Greuther Fürth
Allianz-Arena, Munich
19 Jan, 14:30 Bayer Leverkusen v Eintracht Frankfurt
BayArena, Leverkusen
19 Jan, 14:30 VfL Wolfsburg v VfB Stuttgart
Volkswagen Arena, Wolfsburg
19 Jan, 14:30 Hoffenheim v Borussia M’gladbach
Rhein-Neckar-Arena, Sinsheim
19 Jan, 17:30 Werder Bremen v Borussia Dortmund
Weserstadion, Bremen

No comments:

Post a Comment