VIEW OTHER SITES

Thursday

SIMBA KUWAONDOA MWETA, CHOLLO USAJILI 2013


Klabu ya Simba huenda ikawaacha nyota wake akiwemo beki wa kulia, Nassor Masoud ‘Chollo’ na kipa William Mweta kutokana na ripoti ya daktari wa klabu hiyo, Cossmas Kapinga kuonesha kuwa nyota hao wawili ni wajeruhi wa muda mrefu.

“Ripoti niliyoiwasilisha kwa uongozi nimesema wazi kuhusu wachezaji hao, kwamba ni majeruhi wa muda mrefu, wanaweza kuwa nje miezi zaidi ya mitatu,”alisema Kapinga hii leo.

Taarifa za ndani za klabu hiyo zinaonesha kuwa nyota hao huenda wakatemwa baada ya kupatikana kwa wachezaji wenye uwezo wa kuziba nafasi zao akiwemo Shomari Kapombe ambaye anauwezo wa kucheza kama beki wa pembeni.

“Hawataachwa moja kwa moja, wataendelea kuhudumiwa na klabu, kila kitu kulingana na mikataba yao, ila wataondolewa kwenye usajili, kwa sababu watakuwa wanajaza nafasi wakati hawawezi kucheza. 

Klabu itawahudumia vizuri, wakipona kama mzunguko wa pili au hata msimu ujao, watarudishwa kikosini,”alisema mmoja wa wajumbe wa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment