Mashindano
ya Kombe la Uhai inayoshirikisha timu za chini ya miaka 20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara, yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanziaDesemba 7, mwaka huu kwenye viwanja vya Karume,jijini Dar es Salaam.
Mashindano haya hudhaminiwa na kampuni ya Azam, ambao ni watengenezaji na wasambazaji wa maji ya Uhai, yanatarajiwa kufikia tamati Desemba 22 mwaka huu.
Ofisa
Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura amesema kuwa,
wachezaji watakaoshiriki michuano hiyo ni wale ambao usajili wao umefanyika
TFF na kupatiwa leseni.
“Hakutakuwa
na usajili mwingine wowote mbali na ule uliofanyika sambamba na wa Ligi Kuu.
Taratibu zote za michuano hiyo zitafahamishwa kwa klabu husika ikiwemo ratiba
ya michuano hiyo,”alisema
Mashindano hayo msimu uliopita yalishudia timu ya vijana ya Simba ikitwaa ubingwa kwa kuishinda Azam U20 kwa jumla ya penati 6 - 5.
No comments:
Post a Comment