VIEW OTHER SITES

Monday

Matokeo Ligi kuu bara

Ligi kuu bara

tan

Oktoba 13
Results
13/10/13
Mgambo JKT
Mbeya City
0:1
13/10/13
Mtibwa Sugar
JKT Oljoro
5:1
13/10/13
Ruvu Shooting
Rhino Rangers
1:0
13/10/13
Azam
JKT Ruvu

MILIONI 138 ZAINGIZWA YANGA IKIANGUKIA PUA

Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya wenyeji Azam na Yanga lililochezwa jana Septemba 22 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 138,188,000.
Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo namba 33 la VPL msimu wa 2013/2014 lililomalizika kwa Azam kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 walikuwa 24,020.
Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 33,065,409.1 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 21,079,525.42.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 16,812,919.89, tiketi sh. 5,022,342, gharama za mechi sh. 10,087,751.93, Kamati ya Ligi sh. 10,087,751.93, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 5,043,875.97 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 3,923,014.64.
Mechi iliyopita ya VPL kwenye uwanja huo kati ya Simba na Mbeya City iliingiza sh. 123,971,000.
MECHI YA TOTO, POLISI DOM KUPIGWA J2
Mechi namba 12 ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya Toto Africans na Polisi Dodoma iliyokuwa ichezwe Jumamosi (Septemba 28 mwaka huu) Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza imesogezwa mbele kwa siku moja.
Timu hizo za kundi C sasa zitapambana Jumapili (Septemba 29 mwaka huu) kwenye uwanja huo huo ili kupisha mechi namba 10 kati ya Pamba na Stand United FC ya Shinyanga itakayochezwa Jumamosi (Septemba 28 mwaka huu).
Mechi nyingine za kundi hilo zitakazochezwa Jumamosi ni Mwadui na Polisi Tabora (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga) wakati Kanembwa JKT na Polisi Mara zitacheza kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Friday

KIPLAGAT: SSMB HAIKUPEWA 350 MILIONI NA SERIKALI

Mwenyekiti wa chama cha riadha nchini Kenya (AK), Isaiah Kiplagat amemtaka waziri wa michezo nchini humo, Ababu Namwamba kufuatilia kwa umakini kauli yake kufuatia kauli ya waziri huyo kuwa serikali ya Kenya imetoa shilingi milioni 350 kwa bodi ya usimamizi wa viwanja vya michezo (SSMB).

Kiplagat ambaye ni mjumbe wa bodi hiyo amesema kuwa bodi yake imepatiwa shilingi milioni 70 kwa ajili ya ukarabati wa Kipchoge uliopo Eldoret kutoka kwenye milioni 100 ambazo zilitengwa kwa ajili ya vifaa vya michezo.

Kauli ya waziri huyo imeleta mkanganyiko na bodi hiyo kutokana na ukweli kuwa fedha hizo zilikabidhiwa kwa kitengo cha michezo kinachojihusisha na maendeleo ya miundombinu ya michezo chini ya wizara hiyo na si bodi hiyo.

Kiplagat amesema kuwa waziri wa michezo, Namwamba ameshauriwa vibaya kuhusu zilikopelekwa fedha hizo, na kwamba bodi hiyo imepokea fedha za ukarabati wa viwanja na kuendesha taasisi hiyo tu.

Wawili hao wanadaiwa kukwaruzana wakati wa ufunguzi wa shule ya kukuza vipaji ya Lornah Kiplagat iliyopo Iten, huku Kiplagat akidai kuwa hana mawazo mabaya dhidi ya waziri huyo.

"Waziri hajashauriwa vizuri kuhusu kazi za SSMB na ndio maana alizungumza kitu ambacho hakifahamu," alisema.

Aliongeza kuwa, kwa kaulia ya waziri inamaanisha SSMB haikuumia vizuri fedha hizo kitu ambacho si kweli, na kwamba waziri huyo alitakiwa kupewa taarifa sahihi kuhusu uhusiano uliopo baina ya wizara na bodi hiyo.

Kiplagat alimalizia kwa kusema kuwa hausiki na upotevu wa msaada kamati ya olimpiki ya 2004 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja North Rift, lakini pia akimtaka waziri huyo kutatua matatizo kwa njia ya amani na mazungumzo na si kutumia vitisho

Kiplagat vs Namwamba